Wasanii Wengi wa Kike Wamesahau Kuolewa.:-Wolper

mwanadada Jackline Wolper amefunguka na kusema kuwa watu wamekuwa wakishangaa sana kwa sababu wasanii wengi wa kike siku hizi hawaolewi lakini wanashindwa kujua kuwa hata wanawake siku hizi wamechoshwa na tabia za wanaume na ndio maana wanaona bora kukaa pembeni na kufanya mambo ya muhimu kwanza.

Wolper anasema kuwa wanaume wengi kwa sasa wamekuwa na tabia ya kutumia wanawake  kama njia ya kukuza majina yao na sio kuangalia mapenzi na hicho ni kitu ambacho wanawake wamekiona na wameona waachane nacho.

download latest music    

siku hizi mastaa wengi wameona ni bora kufanya maisha yao na kusahau kabisa kama kuna jambo la  kuolewa ,  na ndio maana unaweza kukaa hata miaka mitano unakuta wasanii wa kike hawajatangaza kuolewa.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.