Wastara Afunguka Kuhusu Kiki za Nusu Utupu.
Mwanadada Wastara Juma amefunguka na kusema kuwa hivi karibuni anategemea kurudi katika maswala ya sanaa baada ya kukaa kwa muda mrefu kutokana na kuumwa kwake lakini hiyo haifanyi yeye kutafuta kiki ili kujirudisha katika sanaa kama wanavyofanya wau wengine.
Wastara anasema kuwa wasichana wengi wamekuwa wakipiga picha za nusu utupu na kuziweka katika kurasa wa mitandao kwa ajili ya kutafuta kiki kitu ambacho kinawapa kiki lakini yeye hawezi kufanya hivyo hata siku moja.
Nina amini kuwa nina mashabiki wengi sana ambao wananipenda sana na sidhani kama watapenda nibadilike na kuanza kuva nguo za utupu kwa ajili ya kutafuta jina kama vijana wa sasa, binafsi sijafikilia kubadilika ili kushindana nao hivyo nitaendelea kufanya kazi zangu kama nilivozoea.