Wastara Alia na Waziri Mwakyembe Kuhusu Pesa Zake

Msanii wa Bongo Movie Wastara Juma maarufu kama Wastara Sajuki amefunguka kuhusu kukata tamaa ya kupata pesa zake anazowadai wachina na kumtaka Waziri Mwakyembe ampe msaada.

Wastara amedai kuwa ameamua kwenda mkoani Dodoma kwa ajili ya kuongea na Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ambaye ameahidi kumsaidia kufuatilia mkataba wake na Wachina anaodai pesa taslimu shilingi milioni 80 za Kitanzania ingawa anaonekana kukata tamaa.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wastara alisema hivi karibuni alifanya mazungumzo na waziri huyo, lakini kwa upande wake amekata tamaa ya kupata pesa hizo kwani mkataba wake na Wachina hao wa Kampuni ya KZG aliokuwa akiwatangazia simu zao ambao umebakiza siku chache umalizike.

Unajua ni siku kama 30 tu zimebaki, naona nimezikatia tamaa, ni Mungu tu atende miujiza nipate pesa hizo. Kwa sasa ninafanya biashara zangu ndogondogo hasa za losheni ambapo nawauzia sana akina mama ili kujikwamua kimaisha kwani kupambania pesa hizo naona nimekwama kabisa“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.