Waziri Shonza Amtuhumu Sista Fey Kwa Kupenda Kiki Kuliko Kazi

Naibu Waziri Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza amemponda vibaya mno msanii wa Bongo fleva Faidha Omary maarufu kama Sista Fey.

Waziri Shonza amemtolea povu zito Sista Fey na kusema kama angeweka jitihada katika kufanya kazi kama ilivyo katika kiki basi bil shaka anagekuwa mbali zaidi.

download latest music    

Shonza alisema hayo usiku wa kuamkia jana alipohudhuria uzinduzi wa mpango wa mwigizaji mkongwe wa sinema za Kibongo, Yvone- Cherry Ngatikwa ‘Monalisa’ wa kuinua vipaji vya filamu kwa wasichana uitwao Mona ACT uliofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar.

Msanii wa kweli ni yule anayejipatia umaarufu kupitia kazi yake na siyo kiki, ukifanya kazi nzuri utapata umaarufu bila hata kiki. Sasa mtu kama Fey mimi siwezi kumuita msanii, inabidi umaarufu uupatie kwenye kazi siyo kiki kila kukicha”.

Sista Fey na sasa mume wake Msanii Hollystar wamejizolea umaarufu Kwenye mitandao ya kijamii kutokana na vituko vyao vya Kimapenzi wanavyofanya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.