WCB walimwa faini milioni 9 na BASATA.

Baraza la Sanaa Tanzania limewatoza faini ya shilingi milion 9 wasanii Diamond Platinumz, Ray vanny pamoja na lebo yao ya wasafi kwa kosa la kukiuka maadili ya baraza hili hasa awalipoambiwa kuufuta wimbo wa mwanza katika you tube channel kabla ya saa 10 siku ya November 12 lakini mapka inafika saa moja wimbo huo bado ulikuwa ukionekana katika channel hiyo.

BASATA ambao walitoa adhabu ya kufumgiwa kwa wimbo huo kutokana na sababu za kinidhamu na maadili ya wimbo huo , na kuwataka wasanii hao kuufuta na kutangaza kutokupigwa katika vyombo vya habari na burudani lakini wasanii hao hawakufanya hivyo badala yake waliendelea kuupigia promo na hata kuupiga katika channel yao.

download latest music    

BASATA wameamuru msanii Rayanny na Diamond kulipa faini ya milion 3 kila mmoja lakini  pia channel ya wasafi pia kutoa milion 3 na kufanya kuwa jumla ya milion 9.Godfrey Mungereza amesema kuwa vyombo vyote vya habari vinatrakiwa kupata taarifa hiyo kuwa wimbo huo kwa sasa haupaswi kupigwa la sivyo faini zitawahusu.

Mkubwa fella ambae ndio meneja mkuu wa wasanii hao anasema kuwa amekubaliana na adhabu hiyo na kupokea maamuzi ya BASATA na kuwataka wasanii kujua kuwa kuna muda wanakuwa wanakosea na kutakiwa kusikiliza wanayoambiwa na wakubwa na viongozi pia.

Mkubwa fela anasema kuwa katika kila mafanikio kuna kuwa na changamoto hivyo wasanii wanapswa kujifunza kukabiliana na kukubali changamoto hizo.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.