Wema Adai Anatamani Kufa, Aamua Kujiondoa Kwenye Mitandao Ya Kijamii

Muigizaji wa Bongo movie mrembo Wema Sepetu amerudi tena midomoni mwa watu baada ya kumwaga povu na kutangaza kuachana na mitandao ya kijamii.

Tetesi za Wema kuhama zimetawala mitandao ya kijamii kwa wiki nzima sasa tangu rafiki yake Steve Nyerere adai Wema atarudi tu CCM ingawa mwenyewe amekataa kuwa habari hizo ni za uongo.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram mchana huu Wema amefunguka na kudai kuwa watu wanamsema sana hivyo amefikia uamuzi wa kuachana na mitandao ya kijamii kwa muda:

Ipo siku ntakufa hakuna mtu anayeishi milele sijui mtaendelea kunisema kwa kejeli na kunitukana matusi ya nguoni au ndiio itakuwa ‘Maskini ya Mungu Dada wa watu alikuwa hivi na vile Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi’ Kuna muda mwingine huwa natamani Subhana Wata’ allah anichukue tu… Ya duniya ni Mengi sana…Kuna muda mwingine nakufuru Mwenyezi Mungu nakutamani nisinge-exist …Ila acha niendelee kumtegemea yeye kila jambo linatokea kwa sababu hili nalo litapita…I think I need time of social media…kwa mara nyingine tena…siwezi jamani….”.

Wema hajaweka wazi sababu gani illiyompelekea mpaka kuandika maneno hayo mazito au ni nani aliyemkasirisha kiasi hicho mpaka kufikia hatua ya kutamani angekuwa amekufa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.