Wema Aingia Katika Majibizano Ya Kisiasa Na Steve Nyerere

Msanii wa filamu Tanzania Wema Sepetu amejikuta akijibizana na msanii mwenzie Steven Nyerere katika mtandao wa instagram baada ya msanii huyo kuandika maneneo ambayo kwa namna  moja ama nyingine yanaonekana kumlenga mwanadada huyo.

Katika ukurasa wake wa Instagram Steven Nyerere aliandika maneno ya pongezi kumpongeza mwanasheria alberto msando kwa  maamuzi yake ya kuamua kuamia katika chama cha CCM hapo jana na kukabithiwa uanachama wa chama hicho mheshimiwa raisi,hata hivyo akiwa kama mmoja wa wanachama wa CCM, Steve Nyerere alimpongeza Albert Msando  lakini pia alisema kuwa kuna msanii mmoja wa kike alikuwa amehama chama hicho anapswa kuiga mfano wake na kurudi kundini .

download latest music    

Ambapo kwa uhalisia wa hivi karibuni , wema sepetu ni moja ya wasanii wa kike walikuwa katika Chama Cha Mapinduzi lakini walibadilisha uelekeo na kuamia kuhama chama hicho na kuamia Chadema.

Hata hivyo baada ya posti hiyo Wema Sepetu alionekana kuguswa na maneno hayo na kuamua kumjibu Steve Nyerere katika uwanja wa komenti na kumwambia kuwa ana imani kabisa kuwa anaeongelewa katika post hiyo sio yeye na kama ni yeye basi hana mpango wowote wa kurudi CCM tena.

HAHAHAA  SASA UTAKUWA MZALENDO WA KWELI ,MSANDO NAESHIMU MAAMUZI YAKO MAANA NI MAAMUZI SAHIHI , KWAKO PAMOJA NA FAMILY YAKO,RAFIKIZAKO,NASI TUPO PAMOJA NAWE,SOON NA YULEEEEEE RAFIKI YETU,DADA YETU MSANII MWENZETU NAYE YUPO NJIANI KUDUDI NYUMBANI ,COMING BACK TIVU,WELCOME MSANDO.

Ambapo baada ya hapo Wema Sepetu alijibu chini yake,

i hope hauniongelei mimi…maana mawazo hayo sina.

Ikumbukwe kuwa Wema Sepetu na mama yake mzazi walitangaza kujiunga na Chadema mwaka huu na kusema kuwa wamechoshwa na siasa za chama tawala.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.