Wema Aingilia Bifu La Zamaradi na Mobetto

Msanii wa Bongo movie Wema Sepetu amejikuta Tena katika headlines za social media baada ya kuingilia kati bifu linalo trend hivi sasa kati ya Zamaradi Mketema na Hamisa Mobetto.

Zama na Mobetto waliingia Kwenye bifu hili baada ya kutifuana kuhusu mshono wa vazi alilovaa Zamaradi Kwenye 40 ya mtoto wake wiki chache zilizopita.

download latest music    

Zamaradi aliandika waraka mrefu wa kurasa tatu ukieleza namna alivyosikitishwa na maneno yanayosambaa mitandaoni kuwa alipewa mshono na Mobeto kwa lengo la kushonewa, lakini akauchukua na kwenda kuushona kwa mtu mwingine huku akimwaga chati zote za WhatsApp walizokuwa wakitumiana.

Lakini pia kwa Mobeto naye aliibuka na kupinga vikali waraka huo. Wakati hayo yakiendelea, Wema kupitia ukurasa wake alinunua ugomvi kwa kuandika; Tuendelee ama tusiendelee’.

Meneja wa Wema, Neema Ndepanya naye hakukaa kimya, aliingilia kati na kumkingia kifua Wema kwa kuandika waraka wake. “Kiki za kuchafuana zilishapitwa na wakati, hakuna kitu kibaya duniani kama kuwa mnafiki, yaani nachukia mtu anajifanya kila wakati anaonewa yeye tu,”

.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.