Wema Auanika Hadharani Ugonjwa Unaomzuia Kuzaa

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu amefunguka na kuweka wazi kuwa taarifa za kukatwa utumbo sio za kweli bali ugonjwa wa gumbo unaomsumbua ndio unamnyima mtoto.

Mwezi uliopita taarifa zilienea Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wema Sepetu anaumwa na yupo hoi kitandani na chanzo cha ugonjwa huo ni kukutwa utumbo ili aweze kupungua.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Gazeti la Risasi, Wema ameanika ugonjwa ambao umekuwa ukimsumbua na kudai ndio unasababisha yeye kukosa mtoto:

Unajua mimi sijakatwa utumbo kama watu wanavyosema; ningekatwa nisingekuwa hivi.

Unajua mimi nilikuwa na tatizo kubwa sana kwa upande wa tumbo langu la uzazi lililosababisha nisiweze kuzaa kwa muda wote huu.

Pia Wema alifunguka jondi ugonjwa huo unekuwa ukimnyima mtoto kwa miaka mingi:

Ngoja niweke wazi leo watu wajue, mimi nina ugonjwa ambao unasababisha mayai yangu ya uzazi kutoboka na kushindwa kupevusha mbegu za uzazi.

Unajua baada ya oparesheni ya India niliporudi nikapata tatizo la kushindwa kupumua vizuri na kingine nikapata maambukizi ya bakteria kwenye kidonda na presha ikawa inashuka.

Naendelea na matibabu lakini tatizo limeanza kupungua nafikiri baada ya mwaka nitakuwa mzima kabisa”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.