“Wema Awe Makini Kuna Watu Wanamuangalia”- Izzo B

Msanii wa muziki wa hip hop nchini anayetokea pande za Mbeya Izzo Business amefungukia sakata lianaloendelea hivi sasa na kushika headlines kwenye mitandao ya kijamii kumuhusu msanii wa maigizo nchini Wema Sepetu.

Wema Sepetu amefikishwa mahakani siku ya jana kwa tuhuma za kusambaza picha zake za faragha na mpenzi wake na kuziweka katika mitandao ya kijamii.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti la Ijumaa, Izzo Business ameibuka na kumshauri Wema kuwa mwangalifu katika siku za mbeleni kwani haileti picha nzuri hasa kwa yeye ambaye ni kioo cha jamii;

Naweza nikasema awe makini sana kutokana na pozisheni ambayo anayo kwa sababu yeye ni brand, anafahamika sana, kuna watu wengi ambao yeye ‘anawa-inspire’ na wengi wanamtazama yeye na kama unavyojua siku hizi kwenye mitandao hadi watoto wa chini ya miaka kumi na nane wapo na wanam-follow Wema kwa sababu wanatamani kuwa kama yeye. Kwa hiyo ushauri wangu ni vitu binafsi kama vile vibaki kuwa binafsi tu, kujirekodi hukatazwi, weka katika sehemu ya siri ili uangalie wewe, lakini siyo mpaka kuvitoa nje siyo kitu kizuri”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.