Wema Sepetu Adaiwa Kumwaga Mpenzi Wake

Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu ametudi Kwenye headlines ambapo anadaiwa amemwaga aliyekuwa mpenzi wake anayeitwa kwa jina la Lawrence Masanja maarufu Kwenye mitandao ya kijamii kama R.A.H.U.R.

Global Publishers wanaripoti kuwa kuvunjika kwa penzi hilo kulitokana na baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa Wema kumng’ata sikio kuwa jamaa aliyenaye hafai na akiendelea naye atakuja kujuta.

download latest music    

Chanzo cha karibu cha Wema kimetiririkia gazeti la Ijumaa Wikienda:

Wema kaamua kumwaga manyanga kwa yule jamaa yake, mwenyewe alishaanza kushitukia kuwa kaingia ‘cha kike’ na hata watu wake walipomtonya kuwa jamaa siyo hakuona ugumu kumtosa. Sasa hivi nasikia ana jamaa mwingine”.

Baada ya Tetesi hizo Gazeti hilo lilimsaka Wema ili kupata ukweli kutoka kwake na alikiri kuwa yeye na mwanaume huyo hawapo wote:

Jamani huyo mtu siko naye na sidhani kama itakuwa ni vyema nikimuongelea kwa sababu sihitaji kufanya hivyo ila kwa kifupi hayupo katika maisha yangu”.

Mahusiano ya Wema yalisemekana kuingia doa wiki chache zilizopita baada video zilizomuonyesha Wema na Diamond wakiwa na ukaribu wa ajabu kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.