“Wewe ni Wangu” Mama Diamond Amfungukia Mumewe

Ikiwa jana ilikuwa ni siku ya Valentine’s Day au maarufu kama Siku ya Wapendanao duniani watu mbali mbali hawakuwa nyuma kuonyeshana mapenzi na Baba wa Kamba wa msanii Diamond Platnumz alimgungukia mkewe.

Ingawa siku ya jana haikuwa nzuri sana kwa Diamond kwani alipigwa kibuti na mama watoto wake mrembo Zarinah Hassan baada ya kumtuhumu kwa tabia ya kupenda michepuko.

download latest music    

Lakini ilikuwa siku nzuri kwa mama mzazi wa Diamond anayejulikana kama Bi. Sandra ambaye siku ya jana alirushwa na mumewe Maisara Abdul Shamte ambaye alimfungukia mazito yaliyo moyoni mwake.

Ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram Shamte alidai kuwa bado anakumbuka siku aliyomuona kwa mara ya kwanza kwa maana ilikuwa ni siku ya furaha kuliko siku zote katika maisha yake alimuandikia Mama Diamond ujumbe huu katika kumtakia Valentines njema:

I still remember the day i met you and smile because it was the happiest day of my life.. meeting you was like listening to the song for the first thing and knowing it would be my favorite, Happy Valentines”.

Baada ya kupewa ujumbe huu na mumewe Mama Diamond hakuona hiyana kujibu kwani alimjibu mumewe kwa kuandika “You are mine, happy Valentines “. Akimaanisha kuwa wewe ni wangu na Valentine njema.

 

Tangu Mama Diamond aolewe  na mumewe huyu ambaye ni Serengeti boy kumekuwa na skendo nyingi za kuwa ni tapeli na kuwa hapatani na mtoto wake wa kambo Diamond habari ambazo familia imekuwa ikizikataa.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.