Wizara Ya Afya Waongelea Picha Ya Utupu Ya Faiza Ally

Baada ya kusambaaa kwa picha ya msanii wa bongo movie Faiza Ally ikimuonyesha yupo leba akijifungua na yeye mwenyewe akionekana kusherekea kutimiza kwa miezi minne ya kujifungua mtoto wake huyo wa kiume wizara ya afya waongelea swala hilo.

Faiza Ally ambae baada ya picha hiyo kupostiwa katika ukurasa wake wa Instagram watu wengi walionekana kutokupendezwa na kitu hicho na kujia juu alionekana kutokujali maneno ya watu  na hata kuingia katika ugomvi na baadhi ya wasanii wenzie kutokana na swala hilo,Hata hivyo picha hivyo ilifutwa baada ya muda mfupi kuwekwa na wamiliki wa mtandao wa instagram kutokana na kuripotiwa kuwa ilikuwa haina maadili kwa jamii na kuwa ilikuwa ikiwadharirisha wanawake.

download latest music    

Kampuni ya  GPL iliamua kuwatafuta wahusika wa afya kuzungumzia swla hilo ambalo kwa namna moja ama nyingine linawza kuwahusu ambapo juhudi za kumpata Waziri wa Afya zilishindikana lakini alipatikana msemaji wa wizara hiyo Ndugu  Nsachris  Mwamwaja na kusema kuwa sio vizuri kitendo kama kile kufanyika na wala hairuhusiwi kabisa , lakini pia hata katika maadili ya kitanzania jambo kama hilo haliwezi kuruhisiwa lakini kwa sababu ameposti katika mitandao ya kijamii, wizara inayohusika na mambo ya mitandao wanatakiwa kufatilia swla hilo.

Lakini kwa kuwa aliweka katika mitandoa ya kijamii basi  watu wa sheria za mitandao wanapaswa kufuatilia swala ilo kwa undani zaidi na kwa namna gani wanaweza kuthibiti swala kama hilo lisiweze kutokea tena. maana ni baya na halifai kabisa.

Hata hivyo mwenyewe Faiza Ally alipotafutwa kuulizwa kuhusu hilo alisema kuwa  kwa iyo picha kwake ni jambo la kawaida tu kwa sabau kila mtu anazaa na kuzaliwa tangu enzi za bibi zeu walikuwa wanafanya kitendo hicho kuhusu kujifunza bado sijajua maana bado sijachukuliwa hatua yoyote ila nina jivunia kwa sababu nimeingia leba.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.