Wolper Adai Hataki Penzi La Mwanaume Ambaye Sio Mtanzania

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali maarufu Jacqueline Wolper amefunguka na kudai hawezi kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na mwanaume ambaye sio Mtanzania.

Wolper ameweka wazi kuwa hawezi Tena kuwa Kwenye Mahusiano na mwanaume ambaye sio Mtanzania kwani alishajifunza siku za nyuma hivyo hawezi kurudia tena.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti la Amani, Wolper alisema kama ni kumpata mpenzi ambaye anaamini atamfaa basi lazima atoke ndani ya nchi yake japokuwa kuna watu walianza minong’ono kuwa alipokuwa nchini Kenya hivi karibuni, alikuwa na mpenzi raia wa nchi hiyo.

Sifikirii kabisa kutoa penzi langu kwa mwanaume ambaye siyo raia wa nchi yangu kwa sasa kwa sababu huko nyuma nilipitia huko lakini sasa sihitaji tena kama nimeamua kupendana na mwanaume basi atakuwa ni wa nchi yangu tu”.

Wolper ambaye kwa sasa aneweka makao nchini Kenya ameshawahi kuwa Kwenye na raia wa Kongo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.