Wolper Afanya Maamuzi Magumu Ya Kuuza Gari Lake

Mbunifu wa mavazi na Muigizaji wa Bongo movie  Jacqueline Massawe maarufu kama Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa Hivi karibuni alifikia uamuzi wa kuuza gari lake.

Wolper ambaye alikuwa anamiliki gari aina ya Toyota Brevis, ameweka wazi kuwa ameamua kuuza gari lake hilo ambalo lilikuwa ndio Usafiri wake pekee ili anunue matirio za kutengenezea magauni.

download latest music    

Katika mahojiano aliyofanya na Mtandao wa Global Publishers, Wolper ameweka wazi kuwa aliamua kuchukua uamuzi wake huo baada ya kupendezwa na matirio hayo alipokuwa nchini Dubai hivi karibuni.

Unajua mimi ni fundi cherehani hivyo  nilivyofika nchini Dubai na kuwaona wadada wakipendeza kwa kuvaa magauni kama haya na nilipowaangalia niliona kabisa kuwa nayamudu kuyadizaini.

Nilichoamua kufanya ni kuuza gari yangu na kwenda kununua matirio haya na kutengeneza magauni kadhaa ambayo kama hili na mengine nayauza. Kwa sasa natumia usafiri wa kukodi na hilo kwangu sioni shida”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.