Wolper Afunguka Kuwaingilia Harmonize na Sarah Tena

Mbunifu wa Mavazi na Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper ameibuka na kujibu Tuhuma Za kuingilia tena mahusiano ya aliyekuwa Mpenzi Wake Harmonize na Mpenzi Wake Mpya Sarah.

Sakata hilo lilijitokeza siku chache zilizopita baada ya Wolper alionekana kuuimba katika akaunti yake ya instagram wa mapensi mabaya akimaanisha ‘mapenzi mabaya’ na yeye kubadilisha na kuimba kinyume.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wolper alisema kuwa amejisikia tu kuimba kinyume kuwa mapensi mazuri.

Lakini watu wanazungumza vingine kwamba namchokoza lakini isivyo hivyo. Nimejisikia tu kuimba haijalishi yeye ndiye ameanza kuimba lakini mimi nikaona niimbe kinyume na yeye alivyoimba ni vile nimejisikia tu kufanya hivyo”.

Baada ya video ile kusambaa watu wengi walichukulia kuwa Wolper amefanya vile ili kumsanifu Sarah hasa kwa sababu wawili hao hawaivi kabisa.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.