Wolper Ajitapa Kuwekewa Ulinzi Mzito na Mpenzi Wake

Msanii wa Bongo movie na mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper amefunguka na kudai kuwa hivi sasa amewekewa ulinzi mkali na Mpenzi Wake kwa sababu ya usalama wake binafsi.

Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa ulinzi mkubwa ambao amewekewa unatokana na Tamasha la Wasafi Festival ambalo anaendelea kushiriki hivyo kila mkoa amewekewa Bodyguard kwa kila mkoa ambao ataenda.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao wa  Dizzim Online Wolper amesema kuwa Mpenzi wake huyo sio mtu wa camera hivyo hawezi kuonekana .

Actually Mr wangu kila mkoa ameniwekea Body Guard na dereva kwahiyo ulimuona Body guard wangu , lakini sio mtu wa camera kwahiyo hawezi kuonekana.

Unajua mikoa tuna wapenzi wengi mtu anaweza akakuhug kama vile kwa Diamond wakachukua cheni, kwahiyo hiyo ndio sababu kubwa kwahiyo sio kwamba unakuja na Body guard kwasababu gani nafikiri hiyo ndio sababu kuu, tunawapenda mashabiki zetu hatutaki kuwakosea“.

Jacqueline ni mmoja kati ya wasanii ambao wameonekana kushiriki katika matamasha yote ya Wasafi Festival katika mikoa mbali mbali.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.