Wolper Atangaza Kuokoka na Kumrudia Mungu

Msanii maarufu wa Bongo movie na mfanyabiashara Jacqueline Wolper amefunguka na kudai ameamua kumrudia Mungu na kuokoka ili aweze kuishi maisha ya wokovu.

Wolper amedai kuwa hivi sasa amemrudia Yesu na kumtumikia kiukweli kweli na kusema anampenda sana Yesu.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers , Wolper alisema ameamua kuokoka kwa sababu anatambua mbali na maisha ya duniani kuna maisha ya mbinguni, kwa hiyo ni vyema akaandaa maisha hayo pia na siyo kujisahau kana kwamba hataondoka duniani.

Kiukweli kwa sasa nimeamua kuokoka na kumrudia Mungu, nina uhakika kwa kufanya kwangu hivi niko kwenye mikono salama na mambo yangu yataninyookea zaidi kuhusu uvaaji wangu siyo tatizo kwa sababu siku hizi tunaokoka kisasa”.

Lakini pia Kwenye Interview hiyo Wolper aneweka wazi sababu iliyomfanya ahamishe makazi yake kutoka Tanzania kwenda nchi ya jirani ya Kenya ni masomo kwani kwa sasa anasomea masuala ya ngozi na urembo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.