Wolper Awashukia Wasanii Wanaoishi Maisha Feki

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo Jacqueline Wolper amewatolea povu mastaa ambao wamekuwa wakidanganya maisha yao kwa kuweka vitu feki Kwenye mitandao ya kijamii.

Wolper amefunguka na kudai huu ndio mwaka wa mastaa hao kutupilia mbali maisha feki feki wanayoishi na kuanza maisha yao ya kihalisia waachane na yale ya mitandao ya kijamii.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Wolper alisema wengi wanajipotosha wenyewe kwa kudanganya maisha waliyonayo, jambo ambalo siyo sawa kwa sababu wanapaswa kubuni vitu vingi vya maendeleo kuliko kujionesha kwenye mitandao kuwa maisha yao ni bomba kumbe hakuna chochote

Hakuna kitu ninakichukia kama maisha ya kuigiza kwenye mitandao ya kijamii, ninayachukia kwa sababu ipo siku mtu atakuja kuona maisha yangu halisi ashangae hivyo inapaswa kila mmoja kuishi vile Mungu amempangia na siyo kuigiza, hayo maisha feki tuyatupe kule”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.