Wolper- Mapenzi na Ali Kiba Yalikuwa Bora Zaidi

Staa wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Jacqueline Wolper ameibuka na kudai hakuna mwanaume ambaye alikuwa mpenzi bora kwake kama ilivyokuwa kwa staa wa Bongo fleva Ali Kiba.

Wolper ambaye siku za nyuma amewahi kukiri kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi kwa muda mrefu na Ali Kiba ingawa hawakuyaweka hadharani na kujulikana na mashabiki.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyiwahi kufanya na East Africa Television, Wolper amefunguka na kuongea haya:

Katika Mahusiano yangu yote ambayo nimewahi kuwa nayo, ambayo naweza kuyapa namba moja na yalikuwa mazuri na ni the best ni yale nilipokuwa na Ali Kiba. Lakini sio kwamba namiss hapana ila tu ninasema yalikuwa Mahusiano bora niliyowahi kuwa nayo”.

Mbali na Ali Kiba, Wolper ameshawahi kuwa Kwenye Mahusiano na mastaa wengine kama Harmonize, Juma Jux na wengineo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.