Wolper: Sina Wivu Nimemualika Harmonize na Mpenzi Wake Kwenye Party Yangu

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo maarufu Bongo, Jacqueline Wolper amefunguka na kudai kuwa hana hata chembe ya wivu wa kimapenzi kwa Harmonize na mpenzi wake Sarah na ndio maana amewaalika wote wawili kwenye party ya birthaday yake.

Wolper na Harmonize waliachana miezi michache iliyopita baada ya kuwa pamoja kwa muda. Baada ya kuachana kila mmoja alimtuhumu mwenzie kwa kuchepuka huku Wolper akiweka wazi kuwa waliachana kwa sababu Harmonize alikuwa na uhusian na Sarah kwa sababu ya fedha alizonazo mzungu huyo. Lakini hata baada ya kuachana na kila mmoja kupata mpenzi ambapo Harmonize alianzisha uhusiano na Sarah na Wolper alianza uhusiano na Brown lakini bado wawili hao wamekuwa na bifu la chini chini.

download latest music    

Siku ya jana ilikuwa sherehe ya siku ya kuzaliwa ya Wolper ‘birthday’ ambapo yeye mashabiki zake pamoja na ndugu zake walienda kushiriki kula chakula cha mchana na kituo  cha kulelea watoto yatima Temeke. Lakini aliweka wazi kuwa party kubwa ya birthday yake itafanyika leo tarehe saba.

Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv, Wolper aliweka wazi kuwa kwa sasa hana tatizo lolote na Harmonize wala  mpenzi wake mzungu Sarah ndio maana amewaalika kwenye sherehe yake:

Nimemualika Harmonize na sio yeye tu hadi mwanamke wake Sarah ili kuonyesha kuwa sina wivu wowote tupo sawa kabisa alafu ningekuwa nasikia wivu kama watu wanavyosema basi nisingewaalika kabisa yaani kwenye maisha mapenzi yanaisha na unatakiwa uendelee na maisha yako sasa mimi nimesha-move on na maisha yangu na nashukuru kwa sasa tumekuwa ndugu na Sarah inabidi tu awe ndugu yangu ili nimsaidie hata kujua kiswahili na pia nimsaidie kama Harmonize akichepuka nimpe nyendo zote ili nimwambie kama anachepuka kwaiyo inafika wakati watu inabidi tu muwe marafiki”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.