Wolper- Sioni Tatizo Kutoka na Lord Eyes

Mbunifu wa mavazi na muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa hana uhusiano na msanii mkongwe wa muziki wa Hip hop nchini Waziri Makuto maarufu kama Lord Eyes.

Kumekuwa na tetesi zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wolper na Lord Eyes wapo kwenye mahusiano ya kimapenzi lakini Wolper amefungukia madai hayo na kusema kuwa hayana ukweli wowote.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wolper  alisema yeye ameona kwenye mitandao taarifa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Lord lakini pia hata siku ikitokea ikawa hivyo sio mbaya kwani sio mwanaume mbaya kwake na pia anavutiwa na jinsi alivyo.

Unajua hata mimi ambaye naambiwa natoka naye nimeona kwenye mitandao tu lakini pia siku ikitokea, freshi tu.Sio mwanaume mbaya maana ana sifa zote za mwanaume ninayempenda au wamesema hivyo kwa sababu niliimba wimbo wake nikauposti mtandaoni ndio tatizo basi ngoja tuone itakavyokuwa maana Wabongo wape picha tu maneno wataweka mwenyewe.” 

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.