Wolper- Wanaume Wengi Wanatumia Wasanii Wa Kike Kwa Kiki

Muigizaji wa Bongo Movie na Mwanamitindo maarufu Jacqueline Wolper ameibuka na kudai ni ngumu kwa Mastaa wengi wa kike kupata wanaume wenye mapenzi ya dhati kwani wengi wao wanataka kuwa nao kwa ajili ya umaarufu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Amani, Wolper alisema kuwa mara ny­ingi wanaume wamewachuku­lia wasanii kama daraja la kusonga mbele au kukuza majina yao lakini siyo mapenzi ya dhati.

download latest music    

Ni hivi mas­taa wengi hasa kwenye tasnia ya uigizaji wameamua kufanya maisha yao wenyewe na kusahau kabisa kama kuna jambo la kuolewa na ndiyo maana unaweza kukaa hata miaka mitano bila kusikia msanii wa kike ameolewa”.

Wolper amekuwa na Mahusiano na wanaume kadhaa ambao kiukweli aliwapa umaarufu wakati wa Mahusiano yao kati yao ni pamoja na staa wa Bongo fleva Harmonize ambaye alijizolea umaarufu sana alipokuwa na Wolper na muziki wake kukua.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.