Yaliyojiri Mahakamani Kwenye Kesi ya Wema Sepetu.

Siku ya jana tarehe 12 march mwaka 2018, Wema Sepetu alionekana tena katika viwanja vya mahakama ya kisutu akiwa na mama yake na watu wake wa karibu kusikiliza kesi yake inayoendelea juu ya madawa ya kulevya iliyoanza tangu mwaka uliopita.

Akitoa ushahidi wa kesi hiyo , mjumbe wa shina  namba 39 anapokaa Wema Septu ametoa ushahidi wa siku ya upekuzi wa kesi hiyo na kusema kuwa siku ya tukio la kupekuliwa kwa nyumba ya Wema Sepetu hakukutwa na bangi bali ilikuwa ni kipisi cha sigara.

download latest music    

Shahidi huyo aliejulikana kama Alphonce  aliyaongea hayo katika mahakama ya kisutu mbele ya Jaji Thomas Simba akisaidiana na wakili wake  Costantine Kakula na kusema kuwa  alikuwepo na alishiriki katika kupekua nyumba ya wema na walikutana na kipisi cha sigara. Alphonce anasma kuwa ingawa haujui bangi ikiwa katika matumizi lakini alishawahi kuona siku moja akiwa mkoani shinyanga ikiwa shambani.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.