Z-Anto Afungukia Tetesi Za Kuoa Mke Wa Pili Kwa Siri

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Ally Mohamed maarufu kama Z- Anto ameibuka na kukana taarifa zinazosambaa kuwa ameoa mke wa pili bila kumtaarifu mke wake .

Gazeti la Ijumaa Wikienda linaripoti kuwa  mwana­muziki huyo hivi karibuni alifunga ndoa na dada wa msanii wa filamu, Wastara Juma aitwaye Naima huku mke mkubwa akiwa hajui, jambo ambalo ni kinyume na utaratibu wa Dini ya Kiislamu.

download latest music    

Mke wa Z-Anto alisema alikuwa anakuta meseji kwenye simu ambazo mumewe huyo alikuwa akiwasiliana na huyo Naima akawa anamuuliza lakini anakuwa mkali, baadaye aligun­dua kuwa walishafunga ndoa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Z-Anto amekataa Tetesi Za kuoa mke mwingine na kusisitiza kuwa taarifa hizo zinazosambaa hazina ukweli wowote.

Niwaambie tu kwamba hizo habari za mimi kuoa hazina ukweli, mimi na mke wangu tuko vizuri kabisa hatuna tatizo ila kama anasema ameenda Bak­wata mimi ndio kwanza nawasi­kia nyie.

Ningekuwa nimeoa ningeweka wazi tu lakini hakuna kitu kama hicho, kuhusu kuwa karibu na familia ya Wastara ni kwamba nil­ianza urafiki na familia hii kama miaka 10 iliyopita, nilikuwa nam­fanyia dua mume wa Wastara marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ alipokuwa anaumwa”.

Kuhusu picha zake na Naima za ndoa zilizosambaa kwenye mitandao, msanii huyo alisema kuna kitu walichokuwa wana­kifanya kuhusiana na sanaa ambacho kwa sasa hawezi kukiweka wazi.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.