Zari Amsamehe Diamond,Wamerudiana (picha ndani)

Ikiwa ni siku chache zimepita tangu sakata la Diamond na Zari lichukue nafasi, baada Diamond kuwa na mahusiano ya siri na Hamisa kufikia hatua ya kumzalisha mtoto na kumkubali mtoto na Zari kutumia mitandao ya kijamii kudai kuwa hajamsamehe hatimaye Zari amemsamehe mpenzi wake.

Tarehe 23 jumamosi ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Zari  ambapo Diamond kwa kupitia ukurasa wake wa instagram aliweka ujumbe huu:

download latest music    

“Uzuri na urembo pengine ningetembea baadhi wanao pia. Lakini akili hekima pamoja na roho yako ya kwenye shida na raha kwangu ndio kitu pekee kinachonifanay nikupende na kukuthamini zaidi kadri siku zinavyozidi kuenda…wanaposema kwenye kila mafanikio ya mwanaume kuna mwanamke imara hawamaanishsi anapika na kuosha vyombo hapaana ni mwanamke mwenyekuwa bega kwa bega na mpenziwe kwenye shida na raha…Happy birthday General”.

Siku hiyo kimya kimya Diamond alisafiri mpaka Afrika ya kusini ambako Zari yupo na kuweka picha mtandaoni akicheza na watoto wao Latifah na Nillan. Baada ya muda waliweka video na picha mbalimbali wakiwaonyesha wapendanao hao wakikumbatiana na kuweka wazi kuwa wamerudiana.

Hizi ni baadhi ya picha kutoka kwa Diamond na Zari:

1. Diamond na Zari wakienda kwenye sherehe ya Zari (Birthday dinner)
2. Diamond akiwa amelala na binti yake Latifah
3. Diamond akiwa anacheza na mtoto wake Nillan (Daddy son moments)

Pamoja na hayo yote yaliyotokea Zari amekiri kuwa ameamua kumsamehe Diamond ili waendelee kulea familia yao ikiwemo watoto wa Ivan, kwani Diamond ameshakuwa baba kwao na pia Diamond alikiri kutorudia kosa tena.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.