Zari: Kamwe Siwezi Kumuanika Mwanaume Wangu Mtandaoni

Mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari’ amefunguka na kuweka wazi kuwa kamwe hatakuja kumuanika tena Mpenzi wake kwenye mtandao.

Baada ya kuachana na Diamond mwaka mmoja uliopita Zari hajawahi kumuweka wazi mwanaume ambaye yupo naye kwenye mahusiano ingawa ameshawahi kusema yupo kwenye mahusiano.

download latest music    
Zari

Zari alifikia hatua ya kuweka wazi hayo alipoulizwa kama kweli hana mpango wa kuolewa na Diamond na atamuanika lini mwanaume anayempenda am­bapo alieleza kuwa mwanaume wake si wa mitandao ya kijamii.

Mume wangu siyo wa social media, ni mume wangu siyo wetu“.

Zari ambaye ana watoto watano wawili kati yao amezaa na Diamond baada ya kuachana na Mbongo Fleva huyo amewahi kuhusishwa kimapen­zi na mwanaume anayeitwa Brian wa nchini Uganda ambapo mara mbili to­fauti alionekana kupiga naye picha za ukaribu lakini mwenyewe alidai kuwa ukaribu wao huo ni wa kikazi tu.

Tangu Diamond aachane na Zari ameshawahi kuwa kwenye mahusiano na wanawake kadhaa ikiwemo mama Watoto Wake Hamisa Mobetto Lakini pia Kim Nana na Sasa mrembo kutoka Kenya Tanasha.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.