Zari na Hamisa Wazidi Kuvurugana Kisa Diamond

Baada ya kumalizika kwa utata wa muda mrefu baada Diamond kukiri kuwa ni baba  wa mtoto wa Hamisa, mashabiki walidhani sakata hilo limeisha na halitasikika tena lakini imekuwa tofauti na matarajio ya wengi kwani picha ndo kwanza kama linaanza kwani sakata hilo limechukua sura mpya.

Zari na Hamisa ambao kwa sasa wote ni mama watoto wa Diamond wameonyeshana chuki kwa kupitia mtandao wa kijamii Snapchat,huku wakiweka wazi  kuwa tusitegemee kuwaona wakiwa marafiki mda wowote kuanzia sasa. Hamisa kwa kudhani kuwa mtoto wake Dylan ameshakuwa na undugu na watoto wa Zari na Diamond Nillan na Tiffah akaamua kuwafata (follow) kwenye instagram kwakutumia ukurasa wa Dyla lakini Zari hakufuraishwa hivo kwa kupitia Snapchat akamwambia Hamisa amuachie watoto wake na wazimu wake unahitaji kupelekwa hodi ya machizi

download latest music    

Kupitia Snapchat Zari aliandika;

“Laki 2 stop following my kids lol, Your obsession needs a mental institution. Like hell?”.

Baada ya kuona hivyo Hamisa ilibidi awa-unfollow watoto wa Zari na kuandika haya kwenye Snapchat;

“Na kama kuna mwanamke mwingine unampenda zaidi yangu…….Bai mwambie mzaa chema shkamoo”.

“Waambie waliopanga mwenye nyumba kaja ndani……Ana meremeta”.

Ingawa watu wengi wangependa kuwaona wanawake hawa wanapatana kwa sababu tu ya watoto wao kwani wote baba yao ni mmoja hivyo wakiwa na maelewano angalau watoto watakua wakijuana kama ni ndugu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.