Makosa Wanayofanya Wanawake Katika Utumiaji wa Vipodozi na Urembo.
Kama ilivyo kote Duniani, kuna makosa yanayofanywa kwenye kutumia vipodozi kwa wanawake Tanzania. Ila kwa sababu tunapenda urembo na tuko kwa ajili ya kusaidiana ni bora kuyaona makosa hayo,yafuatayo ni makosa 10 ya kuweka vipodozi na jinsi ya kuzirekebisha.
Nyusi
Kuna tabia ya wanawake kunyoa nyusi zao sana, na wengine kuzitoa kabisa. Alafu, wanaishia kuzichora na rangi nyeusi.
Hii inamfanya mwanamke kuonekana kama kikatuni, hivyo basi kitu cha kufanya ni:-
- Badala ya kunyoa nywele zote, zipunguze kwa kiasi kidogo
- Usituimie rangi nyeusi kuzijaza. Tumia rangi ya brauni
- Kwa muonekano wa kiasili zaidi, tumia nyusi, poda ya nyusi au gel badala ya penseli.
Tumia faundesheni inayofanana na rangi ya ngozi yako
Ingawa kupata faundesheni inayofanana na ngozi yako ni ngumu, hasa kwa wanawake weusi zaidi, wanawake wengi wanapata shida na kukubali rangi ya kiasili na wanajaribu kutumia vipodozi kubadilisa rangi yao, hivyo ni bora kwanza :-
- Kubali rangi yako ya kiasili
- Rangi yetu inaweza ikawa mweusi au mweupe zaidi kutegemea na msimu. Kwa hiyo ni bora kuwa na faundesheni inayoendana na mabadiliko hayp
Usitumie poda asana
Wadada wengi wamekuwa wakihisi kwamba kutumia poda nying ndio kupendeza zaidi. Matokeo yake, wanaishia kuwa vituko tu , hapa unashauriwa :-
- Tumia poda inayofanana na ngozi yako
- Usiweke poda nyingi. Kiasi kidogo kitakutosha
Matumizi ya kope bandia
Wanawake wengi wanatumia kope bandia zisizo na ubora. Matokeo yake wanafanana na dolli ya mtoto.
Suluhisho:
- Badala ya kutumia kope bandia, nunua wanja nzuri inayonyoosha na kunenepesha kope zako
- Nunua kope bandia zenye ubora (zilizotengenezwa na nywele za binadamu au yalisan.
Eyeshadows
Wanawake wanatumia eyeshadow zinazo ng’aa au za rangi kali. Zaidi ya hapo, hawazichanganyi vizuri.
Suluhisho:
- Tumia eyeshadow za rangi ya dhahabu, brauni au zambarau
- Jifunze jinzi ya kuweka eye shadow vizuri, zikiwemo
- Rangi ya highlighter ya kuweka chini ya nyusi zako
- Rangi ya mpito
- Rangi kuu ya eye shadow
Mdomo
Kabla ya kuweka lipstick, hakikisha mdomo yako inaunyevu. Hii ni muhimu sana kwa lipstick yako kuseti vizuri.
Usiweke vipodozi kwa fujo
Kwenye swala la vipodozi, kutumia kidogo ni bora kuliko kutumia nyingi. Unataka urembo wako wa kiasili kuboreshwa, sio kubadalika kabisa.
Kwa kifupi, ukitumia vipodozi lakini unaonekana kama vile hujatumia vipodozi, basi hapo ndio utakuwa umepatia.