Mambo ya Kuzingatia Katika Kuchagua Nguo za Ujauzito.
Imekuwa ikizoeleka kuwa endapo mama ni mjamzito basi nguo kubwa atakayo kuwa akivaa ni magauni na kujifunga kanga tu, lakini kumbe sio hivyo, Dunia inabadilika na ulimwengu wa fashion unazidi kuendelea hivyo watu kama hawa nao wanapaswa kuonekana tofauti na kuendanana na fashion sio kwa sababu tu ha hali yake.
Hata Hivyo wao pia mabao wamekuwa wabishi na kutaka kuendana na fashion bila kuwa na uchaguzi mzuri wanguo kulingana na hali yao, kwa mfano nguo za kubana sana, viatu virefu sana hii inamuumiza mtoto m, mara nyingine mama mwenyewe lakini pia unaweza kuonekana wa ajabu zaidi kwa sababu unashindwa kuzuia hisia zake kuendana na fashion.
Katika kuchagua nguo nzuri za wakati wa ujauzito unaakiwa kwanza:-
Kulikubali umbo lako.
kadri tumbo linavyokuwa na umb lako linaongezeka hivyo unapswa kutambua kuwa umbo lako sio kama pale mwanzo hivyo hata nguo zako zinabidi kuendana na hilo, nunua nguo ambazo hazibani , zenye kupitisha hewa kwa uraisi zaidi .
Usibadilishe mtindo wako wa kawaida.
kama ulikuwa unapendelea sana kuvaa magauni haina haja ya kubadilika kwa sababu ya hali yako ya ujauzito na kuanza kuvaa nguo zingine, angalia tu kuwa kama ni jinsi au sketi ndio umezoea kuvaa basi tafuta zile zenye kuipa nafasi hali yako na sio kubadilika kabisa.
Nunua vifaa vya mitindo.
Achana na habari ya kubwetea tu na kuonekana wa kawaida sana, vaa na nunua vitu kama hereni, bangili, saa na vitu mbalimbali vya mitindo na mapambo kupendezesha muonekano wako.
Nunua nguo za rangi.
Kuna nguo ambazo zinatoa mwanga mzuri kwa mama mjamizto kwa kuzingatia pia na hali aliyonayo, jaribu kununua nguo zenye rangi ya kungaa ili kuonekana mrembo zaidi.
KUMBUKA:-Kuwa mjamzito sio mwisho wa kuwa mrembo, wengi wamekuwa wakijiweka kihasara hasara kwa sababu ya hali zao , Urembo wa mwanamke ni muda wowote na hii inaendelea hata baada ya kujifunga na wakati wa kunyonyesha.