Barakah the Prince amjibu Ben Pol baada ya kudai walimpunguza kwenye show

Msanii kutoka Tanzania Barakah the Prince amefunguka kwa mara ya kwanza kumjibu Ben Pol ambaye alidai hivi karibuni kuwa msanii huyu alipunguzwa kwenye show ambayo alitakiwa kutokea na wasanii wenzake Kama Juma Jux.

Akizungumza kwenye interview mpya na kipindi cha XXL cha Clouds FM Barakah alisema kuwa wake Ben Pol alichozumgumzia kwenye interview yake ni uongo, huku alisema;

download latest music    


“Mimi sipunguzwi, nilijitoa nikawaambia nina menejiment ambayo ina utaratibu wake, ninapofanya kazi lazima kuwe na makubaliano na mkataba kwa sababu wao walishindwa kufuata utartibu nikajitoa kwenye hiyo show yao.”

Aliendelea kwa kusema,

“Hatukuwa na muungano wowote kusema kwamba tulikuwa na tour, tulifanya show moja tu ile, show iliyofuata uongozi wangu ukataka utaratibu wa hizo show waliposhindwa nikawaambia mimi sitaweza kufanya. Sema nyimbo yake ni mbaya asitafute sababu ya kujitetetea… utovu wa nidhamu yule (Ben Pol) baba yangu?”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua