Dada wa Diamond Amtaka Diamond Amsaidie Baba Yao Maana Ana Hali Mbaya

Mwanamke mmoja aliyejitambulisha kama Dada yake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, anayejulikana kwa jina la Zubeda amempigia magoti Diamond amsaidie baba yake ambaye anaumwa hoi.

Dada huyo ambaye wakati akiwasili nchini alipokelewa na Baba mzazi wa Diamond, mzee Abdul Juma, amesema hajui kipi kibaya ambacho baba alimkosea Diamond hadi kufika hatua ya kuwa mbali naye na kutomsaidia ilihali ni mgonjwa sana akisumbuliwa na tatizo la miguu kuvimba kwa muda mrefu.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Zubeda amemtaka Diamond akubali kuonana naye ili waongee na amwambie kwanini amemtelekeza baba yake kwani ni mgonjwa sana na anahitaji msaada wa hali na Mali.

Nimetoka London nimekuja Tanzania kuonana na Diamond na kumuuliza Mzee Abdul amemfanya nini Mpaka hutaki kumuona wala kumsaidia Baba yake kwani kiukweli Baba yake anaumwa sana anahitaji msaada”.

Lakini pia Mwanamama huyo amesema kuwa yupo tayari kusaidia kumaliza tofauti zilizopo kati ya Diamond na Baba yake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.