Dully Sykes Afunguka Kukopiwa na Harmonize

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Abdul Sykes maarufu kama Dully Sykes amefunguka na kuweka wazi kuwa amefurahi Baada ya Msanii Harmonize kukopi nyimbo yake.

Harmonize ametumia melody ya wimbo Dully Sykes wa muda mrefu unaofahamika kama ‘Handsome’ katika wimbo wake mpya alioutoa wa Kainama na kusema amefurahi kwa sababu ameona kama amemuenzi.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Dully alisema kabla Harmonize hajaweka maneno katika wimbo huo, alimshirikisha kwanza na hata wakati anarekodi alikuwepo studio na akamshauri baadhi ya vitu.

Wala sijachukulia kama kaniibia melody yangu ila nimechukulia kama hali ya kunienzi f’lani hivi kwa nilichokifanya huko nyuma nilifurahi sana alipotoa wazo la kuchukua melody hiyo ambayo nilitumia katika wimbo wangu wa zamani uliokuwa unafahamika kama Handsome, na ameutendea haki vilivyo nimefurahi sana”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.