Mr. Blue: Kuanzia Leo Sitaki Tuzo Yoyote Kutoka Tanzania

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Mr. Blue amefunguka na kusema kuwa anaumua sana kuwa mpaka leo hii na ukongwe wake kwenye gemu lakini hana tuzo hata moja lakini pia amekiri kuwa kuanzia leo hataki tena Tuzo kutoka Tanzania.

Mr. Blue ni moja kati ya wasanii wachache waanzilishi wa mziki wa Bongo fleva ambaye alianza kuimba tangu enzi hizo mziki huo unaanza anza lakini cha kusikitisha msanii kama huyu mpaka leo hii hana tuzo hata moja ya hapa nchini wala ya nje ya nchi.

download latest music    

Mr. Blue amefunguka keen he mahojiano na Planet Bongo ya East Africa na kuelezea jinsu alivyokatishwa tamaaa kwa muda mrefu na uamuzi alioamua kuchukua juu ya hilo:

Kusema kweli huwa nafurahi nikipita mtaani naona bado heshima ipo kutoka kwa mashsbiki wa kweli lakini naumia sana ninapo ona sina tuzo yoyote kabatini mpaka leo alafu ninachoumia sio kukosa tuzo peke yake pia kuona mpaka leo hwajanitafutia category ya muziki ninaofanya kwa sababu ukizungumzia marapa wanaofanya hip hop Tanzania mimi siwekwagi kwenye bongo fleva swekwi sasa moans najiuliza mimi ni nani mpaka najiona nipo tu. Kwaiyo kuanzia sahivi sikubali Tuzo yoyote kutoka Tanzania yaani nikipewa nakataa ila Tuzo za nje ya nchi poa tu”.

Hivi sasa Mr. Blue anatamba na wimbo wake wa ‘Mbwa koko’ uliofanikiwa kukamata chati kwenye mtandao wa YouTube na kupelekea kuwa namba moja kwa muda wa wiki nzima.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.