Muigizaji Elizabeth Michael akana taarifa za ndoa yake na Majay

Elizabeth Michael hivi karibuni alikuwa anasemekana kuwa anatarajia kufunga ndoa na mpenzi wake Majay ambaye pia ni bosi wa EFM na TVE. Taarifa hii ilienea baada ya magazeti kadhaa ya Tanzania yalioandika kusema kuwa walifanya mahojiano na mrembo huyo.

Hata hivyo Elizabeth Micheal anaejulikana kama Lulu amekana taarifa hizi kupitia mtandao wa Twitter baada ya kuandika ujumbe uliosema…

download latest music    

“Hivi kwa Akili yenu Ndoa inatangazwaga Kwenye Magazeti!??Muwege mnajiongeza kabla ya kuparamia Story…!.”

Hii inakuja baada ya gazeti la Mtanzania lilikiri kwa kumnukuu muigizaji huyo…

“Siku zinakaribia na karibu tarehe ya ndoa yangu itatangazwa kwa uwezo wa Mungu. Hapo ndipo waliotamani tuachane wataziba midomo, maana natarajiwa kuwa mke halali hivi karibuni.”

Kwa hivi sasa inaonekana kuwa Lulu hana mipango ya kuolewa.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua