Ni nini kinachoendelea kati ya Alikiba na Ruby?

Image: Alikiba

Ubuyu mtaani ni kuwa Alikiba na Ruby kuwa wamekuwa watu wa karibu sana na kuzua maswali mitandaoni ya kijamii.

Habari hii imevuma mda mchache baada ya Alikiba alisemekana kuwa alimvisha pete ya uchumba mwandani wake aitwaye Amina kutoka nchini Kenya.

download latest music    
Ruby
Ruby

Hata hivyo baada ya kuonekana na Ruby sana wengi wanaamini kuwa wawili hao wanauwezekano wa kuwa wapenzi ikiwa hawafanyi wimbo mpya pamoja.

Ruby ambaye aliweza kuzungumzia jambo hili aliwasihi watu hataki kuulizwa kuhusu mahusiano yake…. Ruby alisema,

“Sorry, sitaki kuulizwa kuhusiana na hayo mambo, naomba niulizwe kuhusu kazi zangu tu!”

Alikiba naye hajazungumzia jambo hili kwa sasa hata hivyo kuna uwezakano kuwa yeye na Ruby wanapanga kuachia wimbo mpya hivi karibuni.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua