Staa wa filamu ya Bongo Kajala Masanja afunguka kuhusu yeye kutumia bangi

Utumiaji wa bangi umepigwa marufuku Tanzania, hata hivyo bado kuna baadhi ya watu mashuhuru ambao wanatumia ama wamewai tumia bangi.

Wema Sepetu ako na kesi kotoni ambayo anashtakiwa kwa kosa la kukutwa na bangi. Mrembo huyo alikamatwa na kuwekwa korokoroni kwa siku sita baada ya polisi kumshika na bangi Februari mwaka huu.

download latest music    

Sasa nyota mwingine wa Bongo movies pia amefunguka kuhusu utumiaji wa Bangi, Kajala Masanja alisema aliwai tumia bangi miaka kadhaa zilizopita.

Katika mahojiano na Bongo Movies, Masanja alieleza kuwa alijikuta mikononi mwa marafiki waovu waliojihusisha na utumiaji wa bangi na kusababisha yeye pia kutumia bangi.

“Unajua inafika mahali sisi kama vioo vya jamii inatupasa kuzungumza ukweli wa maisha yetu husasan ya nyuma, ili kama ni watu kujifunza iwe hivyo, binafsi nimewahi kupitia maisha ambayo naweza kuyaita ya mpito, kipindi ambacho kila mtu hupitia katika harakati za ukuaji, kwamba nilijiingiza kwenye kampani za marafiki ambao ni watumiaji wa bangi.

“Hivyo, walinishawishi na kujikuta nikijiingiza kwenye ulevi huo, kidogo nipotee ila namshukuru sana Mungu kwani sikuwahi kuvuta madawa mengine kama cocaine, heroine sijui kujidunga masindano na mambo mengine ya kufanana na hayo, lakini ukweli kabisa huwa najuta sana kwa kuvuta bangi,” alisema Kajala Masanja.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere