‘Wengi walikushauri utoe mimba yangu lakini nakushuru kwa kunipa mtoto’ Rayvanny amwandikia mchumba wake ujumbe huu

Image: Rayvanny na mchumba wake

Rayvanny na mchumba wake wamebarikiwa na mtoto wa kiume, Jaydan. Taarifa za kupata mtoto zilitolewa na Rayvanny kupitia Instagram.

Muimbaji huyu wa Wasafi alimpongeza mchumba wake kwa kumuandikia ujumbe ambao umeewacha wengi wakitamani mapenzi yao. Hata hivyo, Rayvanny aliweza kuweka wazi kuwa wengi walikuwa wakimsihi Fahyma kutoa mimba yake kwa sababu ya umri wake mdogo.

download latest music    

Lakini kwa sababu aliamua kuiweka na kuzaa Rayvanny amemfungulia roho kupitia instagram na kuandika kusema….

Rayvanny na mchumba wake
Rayvanny na mchumba wake

Kuna Kuachana, kugombana,kutengana lakini kuacha yote hayo Swala Kubwa Sana Ulilolifanya Ambalo sitoweza kulisahau ni Kunipa @jaydanvanny kwenye maisha yangu.Maana Ungweza Kutoa Mimba lakini Ulikua Na nia njema na mwanao .Wengi walikushauri Utoe wakasema unajiharibia Future wakasema bado mapema lakini haukua tayari kumpoteza Mwanao. @fahyma_ @jaydanvanny We love you son #Youngparents?

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua