Z Anto: Sina haja ya kushindana na Diamond na Ali Kiba

Z Anto amegonga vichwa vya habari kwa kutoa madai ambayo imewatikisha mashabiki wa Diamond Platnumz na Ali Kiba.

Mwimbaji huyo ambaye alivuma kwa ngoma yake kali – ‘Binti Kiziwi’ amekiri kuwa Diamond na Ali Kiba ndo mabingwa wa muziki wa Bongo lakini ako na uhakika kuwa atawaangusha kumuziki.

download latest music    
Z Anto

Z Anto alifunguka kuhusu mpanga wake ya kuwabwaga Diamond na Aki Kiba akiongea na Bongo5. Alisema kuwa haitaji kushindana nao kwani muziki wake utapita katikati yao na kunawiri kuwashinda.

“Mimi ni mkongwe kwenye huu muziki na bado nina nafasi ya kufanya mambo makubwa zaidi. Najua kwa sasa Diamond na Alikiba ndio wasanii wanaozungumziwa zaidi lakini mimi sina haja ya kushanda nao muziki wangu nitaupitisha katikati yao,” alisema Z Anto.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere