Fanya Yafuatayo Na Utaonekana Mrembo Siku Zote

Kila mtu amekuwa na dhana yake tofauti katika kutasfiri dhana ya urembo.kuna wanajua kuwa ili kuwa mrembo basi ni alzima uwe na ngozi nyeupe au nywele ndefu au umbo lako liwe la kuvutiwa .Lakini sio kweli, urembo ni vile wewe unajiweka ili  kuwa nadhifu na kuwa na muonekano wa kuvutia hata kama uwe mwembamba kiasi gani au mweusi kiasi gani.

Kwanza jiaminishe kuwa wewe ni mrembo kuliko watu wanavyokuchukulia alafu kisha fanya yafuatayo:

download latest music    

1:Safisha ngozi yako kila siku.

katika kusafisha ngozi kuna mambo mengi ,jitahidi kuifanya ngozi yako kuonekana nyororo na safi muda wote, hii itakusaidia kuonekana mrembo kwa asilimia zote.Ondoa ngozi iliyokufa , sugua ngozi ili kuondoa mafuta na uchafu unakuwa umeganda katika ngozi yako.Hii inaweza kufanyika kwa masaage au kufanya scrub mwili.

jaribu kuchangua bidhaa bora za kutumia katika kusafisha ngozi yako.usizisahau nywele zako kila wakati, zitunze  na uzipende hata kama ni fupi.Jua kabisa urembo sio sura tu bali kila sehemu ya mwili wako inapokuwa safi inarekebisha muonekano wako.

2.Fanya mazoezi

Mazoezi yanakufanya uwe mkakamavu siku zote , lakini pia mazoezi yanasawazisha mwili na kufanya uwe na umbo la wastani  lenye muonekano wa kuvutia.Katika vitu vinavyochangia afya ya ngozi na urembo mazoezi pia ni msaada mkubwa sana.Fanya mazoezi kuwa ni ratiba yako ya maisha.

3.Epuka vipodozi vya mara kwa mara.

Kuna watu wamezoea kupaka vipodozi kila muda, wanafanya ngozi muda wote kuwa imefungana na kukosa hewa ya kutosha.sio kila kipodozi ni urembo vingine uharibu ngozi yako.Onana na wataalamu wakupe ushauri juu ya kipodozi sahihi cha kutumia,lakini pia epuka kupaka vipodozi na ukalala navyo hii ni mbaya zaidi.

Mara nyingi vipodozi vyenye kemikali viansababisha kulegea kwa ngozi, lakini pia vile vinavyochubua ufanya wanawake wengi kushindwa kushonwa wakati wa  kujifungua hasa kwa wale wanahitajika kufanyiwa operation,ngozi kuungua na kushindwa kukaa juani.

4.Jitahidi kupata usingizi wa kutosha

Sio kwa afya ya mwili na akili tu , badi usingizi wa kutosha usababisha mtu kuonekana mrembo, kulala kwa muda unaofaa kuna kufanya usionekane  mchovu na macho yako yanakuwa angavu siku zote.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.