Mambo Nay wa Mitego na Waziri Mwakyembe walizungumzia baada ya kukutana

Hivi leo Nay wa Mitego alikutana na waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Dr. Harrison Mwakyembe ambapo walizungumzia mambo mbalimbali.

Nay amekuwa akizungumziwa kwa muda sasa na ni baada ya kukamatwa na polisi kwa ajili ya wimbo wake wapo ambao ulionekana kukashifu serikali ya Magufuli.

Alikuja kuachiliwa baadaye kwa maagizo ya waziri Mwakyembe na leo walikutana kuongelea mambo tofauti ikiwemo mambo wanafaa kuongeza kwenye wimbo huo.