Nipo Tayari Kuzaa Mtoto Mwingine na Steve Nyerere-Wellu

Msanii wa Bongo movie Wellu Sengo amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kuzaa na mzazi mwenzake Steve Nyerere ambaye tayari amezaa naye Mtoto mmoja.

Mwaka jana uhusiano wa Steve Nyerere na Wellu Sengo ulitengeneza headlines Baada ya kuwekwa hadharani Baada ya kufanyika kwa siri kwa muda mrefu hasa kwa sababu Stevw alisemekana kuwa na mke mwingine.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti Ijumaa Wikienda, Wellu alisema kuwa amefurahi kuwa mama na anap­enda sana watoto hivyo anategemea kuongeza mtoto mwingine na Steve Nyerere kwani ana malengo ya kuzaa watoto wanne.

Kwa jinsi nnavyo­tamani na kupenda watoto nitaongeza mtoto mwingine soon na malengo yangu ni kupata watoto wanne hivyo namuomba Mungu anikamilishie malengo yangu“.