Zari Awashukuru Mashabiki kwa Kufikisha Followers Milioni 4,Apanga Kujenga Clinic ya kina Mama

Kwa mara ya kwanza mwanadada Zari the bossy ameweka picha yake iliyotumika katika video ya wimbo mpya wa diamond iyena , video ambayo ime-trend sana na kusababisha wawili hao kurudiana baada ya mashabiki kumpigia kelele sana Babu Tale kwamba wanaomba kufanya usukuhishi wao.

Katika picha hiyo, Zari the bossy aliandika maneno ya kuwashukuru mashabiki wake kwa kumfuata kwa wingi mpaka kufikisha followers  million 4  katika mtandao wa instagram .

Zari anaingiakatika list ya wanawake wachache wenye ushawishi mkubwa  katika mtandao hasa wa instagram na pia amekuwa moja ya wanawake waliopo nje ya Tanzania lakini wanaopendwa sana na watanzania.

katika ukurasa wake aliandika”wapendwa wangu sina cha zaidi cha kuwalipa zaidi ya kusema asanteni sana,ninyi ni mandugu kwangu mmekuwa bega wa bega  kwenye shida na raha sasa mnichangie $ 1 ili tujenge clinic ya wanawake dar,najua tukipata baba magufuli atatupa kiwanja tu  PENDA SANA NYINYI, THANK YOU SO MUCH.”