Urembo Kipindi cha Ujauzito na Baada ya Kujifungua.

Kipindi cha ujauzito wanawake wengi hujikuta wakiwa katika hali ya  kuchakaa kwa sababu ya hali zao.wengine ujikuta wakijiendekeza hata kufikia hatua ya kukatwa nywele au kutovaa vizuri kisa tu yeye ni mama mlezi wa mimba.Ukweli utabaki kuwa  sifa kuu ya mwanamke ni kuonekana msafi nadhifu na mwenye kuvutia siku zote.

Hali  hii ya kutokuwa nadhifu uweza kuendelea hata baaada ya kujifungua tena huku uweza kuwa mbaya zaidi kwa sababu mama anakuwa yuko busy sana na mtoto na hapaswi kupaka baadhi ya vitu vinavyoweza kumuathiri mtoto wake.

download latest music    

Mimba au mtoto haiwezi kuwa sababu kubwa ya mama kutokuwa mrembo, jukumu kubwa ni kubaki na muonekano wake ule ule wa zamani na ikibidi kuzidisha kwa sababu ni sifa ya kike.lakini urembo huu unapaswa kuzingatia zaidi upakaji wa mafuta au vipodozi ambavyo havina kabisa kemikali au harufu mbaya kwa mtoto anayemnyonyesha.

Kuna baadhi ya mazoezi pia yanaweza kusaidia kurudisha urembo na umbile lako lisizidi lilivyokuwa hapo awali, pia zingatia kula vyakula vya wastani kwa sababu wazazi wengi hujikuta wakijiachia na kula hovyo kwa kisingizio cha kuwa wananyonyesha.

Jaribu kuwa na nywele safi  ambazo  hazitakuwa zikimsumbua mtoto wako lakini pia pia usiwe unatumia muda mwingi kwenda saluni na kusababisha kukosa muda mwingi wa kukaa na mtoto kwa kipindi hicho, kwa upande wa kucha hakikisha kucha sio ndefu na usipende kupaka rangi kwa sababu wewe unatoa huduma kwa mtoto.

Kitu kikubwa cha kujitahidi ni kulinda muonekano wako wa ndani na wa nje na sio kuzaa kukufanye ubadilike uwe mtu mwingiene kabisa asiyejipenda na kujijali hata kidogo.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.