Vanessa Mdee Amwaga Povu Kwa Mashabiki Waliosema Hajapendeza na Staili Yake ya Nywele

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri hivi sasa na albamu yake ya Money Monday’s Vanessa Mdee amejikuta akiingia kwenye trend ya mastaa iliyoingia hivi sasa ya kubleach nywele.

Vanessa ameungana na mastaa wenzake kama Ali Kiba na Ommy Dimpoz walioonyesha staili yao mpya ya nywele wiki hii mwanzoni ambapo pia walionekana rangi walizopaka kwenye nywele ambapo Ali Kiba alikuwa amepaka rangi nyekundu na Ommy Dimpoz alikuwa amepaka rangi ya njano.

download latest music    

 

 

Vanessa alionyesha staili yake mpya siku ya jana kupitia mtandao wa Instagram ambapo alikuwa amepaka rangi ya machungwa (orange) ambapo alisindikiza picha hiyo na ujumbe uliosema:

New hair who is this? Benpol najua utakuwa umefarijika sana”.

 

Lakini baada ya picha hizo kusambaa mtandaoni Vanessa aliwatolea povu zito mashabiki zake waliokuwa wanamsema kuwa hajapendeza na rangi ile ambapo kupitia mtandao wa Instagram alimwaga povu hili:

Tatizo la wengi mmekariri kila kitu hadi nywele mnataka kunipangia nikiwa na nywele za kuvaa mnasema nikivua mnasema sasa nasemaje Ben amefarijika”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.