Alichosema staa wa filamu Bongo,Lulu kuhusu ‘kuachana’ na mchumba wake

Stori za mitaani kuhusu uchumba wa Elizabeth Michael,ajulikanaye kwa jina Lulu,mkali wa filamu Tanzania,kukatika zimemkwaza na kumpandisha hasira sio mchezo.

Inaripotiwa kua sio mapenzi mubashara tena kati yake na mpenzi wake,baada ya wawili hao kutemana kama big G.

download latest music    
Elizabeth Michael na Majizo

Kwa mujibu wa taarifa hii,mambo sio kama kawaida kwani pendo limevunjika huku kila moja akiongea lake.

Madai kuwa staa huyo wa filamu na mpenzi wake kuonyeshana kisogo yalienea kwenye mitandao ya kijamii huku wadaku wa town wakiongeza makali na pilipili zaidi na kudai kuwa, Lulu karejea nyumbani kwao na ana mpango wa kuanzisha maisha yake upya.

Staa huyo amekereka kuhusu stori hii,haya ndio maneno yake kwa wanahabari wanaotaka kujua kulikoni.

“Sitaki kuongelea chochote…sitaki kuongelea chochote, pliz…unajua mimi siyo mtu wa magazeti kabisa na unanijua vizuri…” amesema Lulu.

Kumbe hapendi stori za magazeti?

About this writer:

Irari Ngugi

Lover of life, lover of big boobs and certified celebrity squasher. Catch me if you can on facebook as Irari Ngugi