Baada ya kufanya collabo na King Kiba, Barakah The Prince aeleza changamoto alizopitia

Image: Barakah The Prince

Mwimbaji wa Tanzania Barakah the Prince ameeleza baadhi ya changamoto alizopitia baada ya kutoa colabo ya wimbo wake Nisamehe aliyomshirikisha King kiba. Hii ni kufuatia tofauti zilizopo kati ya team Kiba na team Diamond Platnumz.

Akizungumza katika interview na kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha Salama Jabir, Barakah alisema kuwa ilikuwa vigumu kupata support kutoka team Diamond ambao hawampi support Kiba.

download latest music    

Ujue Alikiba ni brand kubwa na ni brand ambayo ina mvutano na vitu vingi, kwahiyo unavyofavya collabo na Alikiba kuna mawili hapo, kuna nyimbo kufanya vizuri na kuna nyimbo kufanya vizuri wastani, wa kawaida kwasababu ya ule mvutano wa kibiashara ambao upo kati yake na timu nyingine

Ingawa halalamika kuwa jambo hili liliadhiri wimbo wake, muimbaji huyu amekiri kuwa timu hizi mbili zinangumvu ya kuaffect career ya muimbaji bongo. Kwa hivi sasa anaendelea kuzipush nyimbu zake kabla atoe project nyingine mwaka huu.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua