Barakah The Prince awararua mashabiki wake ambao walimuita msaliti

Barakah The Prince hatambui kwamba mashabiki wake ndo wanachangia yeye kufauli kimuziki – mwimbaji huyo alikerwa sana baada ya kuitwa msaliti.

Siku chache baada ya kuonekana kwa picha na Babu Tale ambaye ni meneja wake Diamond Platnumz, baadhi ya mashabiki wake walimkosoa kwa kile walitaja kama usaliti.

download latest music    
Babu Tale na Barakah The Prince

Barakah The Prince na Alikiba wako katika lebo inayoitwa Rock Star 4000. Mashabiki wa Barakah walimwita msaliti kwasababu Diamond and Alikiba ni maadui.

Hit maker huyo hata hivyo hakufuraishwa kuitwa msaliti, aliwaonya mashabiki wasimpangie maisha yake binafsi. Aliwaambia kwamba wao kinachowahusu kutoka kwake ni muziki mzuri tu.

“Wewe kama ni shabiki wangu wa muziki haimaanishi pia ni shabiki wa maisha yangu binafsi, maisha yangu binafsi mniachie. Shabiki wewe ni nani sasa mpaka unipangie maisha? kama mtu niliyepiga naye picha ni binadamu siyo shetani lakini cha ajabu mashabiki ndiyo wanaonitukana na kuongea hivi na vile wakati uongozi wangu haujasema kama nakosea,” Barakah The Prince alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio.

 

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere