Dadake mdogo Vanessa Mdee asimulia changamoto alizopitia kabla ya kuwa maarufu

Image: Mimi Mars

Mimi Mars ambaye ni dadake mdogo Vanessa Mdee hivi karibuni aliweza kufunguka kuhusu changamoto alizopitia kabla ya kuwa muimbaji maarufu bongo. Kama wasanii wenzake alitafuta njia za kuiingia kwenye movie za bongo lakini hakuwa na uwezo.

Akizungumza kwenye kipindi cha Bongo Dot Home cha Times FM, Mimi alisema kuwa dadake mkubwa Vanessa aliweza kumsaidia awezavyo na ata kutafuta usadizi kutoka kwa Lulu na Wema Sepetu kumpa shavu dadake lakini waliambulia patupu.

download latest music    

Hata hivyo Mimi Mars hana kinyongo na wasanii hawa kwani anaamini kuwa wakati wake haukuwa umefika. Katika interview yake Mimi alisema kuwa sasa hivi yeye na akina Wema ni marafiki wakubwa na ingawa hawakuwepo alipokuwa akiwahitaji, bado anawachukulia kama marafiki wa dhati.

“Nilishawahi kumuomba Lulu, Elizabeth Michael nakumbuka tuliwahi kuongea naye hata akina Wema kuomba kuingiza kwenye bongo movie lakini, Vanessa ndio alikuwa ananisaidia kuongea nao lakini kama walinipiga chini fulani hivi but it’s okay,”

Hivi sasa Mimi Mars anafanya vyema na wimbo wake na akona matumaini ya kwenda mbali kama dadake. Tazama interview yake hapa chini.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua