Diamond amrai Ali Kiba kuweka muziki wake wasafi.com

Akiongea kwenye mahojiano ya kipindi cha 360 cha Clouds FM, Diamond Platnumz alikiri kwamba hana tatizo na Ali Kiba. Diamond na Kiba wamekuwa na beef zito sana kwa takribani miaka mitatu.

Diamond aliambia Clouds FM kwamba anaheshimu Ali Kiba, alifunguka na kusema kwamba uongozi wake uko katika mazungumzo na uongozi wa Ali Kiba ili Kiba aweze kuuza nyimbo zake kwenye mtandao wa wasafidotcom ambao ni mradi mpya wa Diamond.

download latest music    
Ali Kiba and Diamond TBT

Baadaye usiku kupitia akaunti yake ya Instagram, Ali Kiba aliandika caption zenye utata zilizotafsiriwa na mashabiki na wadau mbalimbali kuwa zimelenga kujibu maneno hayo ya Diamond Platnumz.

“Waambie Wasituzoee kabisa MAZOEA kuzoeana ?? @billnass #alikibaworldtour2k17 #KingKiba,” Ali Kiba aliandika.

Watu wengi wanaamini kwamba Diamond anahitaji amani na Ali Kiba kwasababu za kibiashara zaidi. Iwapo Ali Kiba atakubali kuuza wimbo zake wasafi.com, Diamond atafaidika zaidi kwasababu Ali Kiba ako na wafwasi wengi.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere